SIKU YA KWANZA

Baba Yosefu, ulimfundisha Yesu jinsi ya kusali, kucheza na kufanya kazi, utusaidie kutambua kwamba tunaweza kupata elimu kwa kusikiliza na kujifunza. Tukiwa na wewe ambaye unatusaidia na kutuongoza, tunaomba, ee Mt. Yosefu, utuombee tuchague njia sahihi na tubaki kuwa waaminifu katika mafundisho ya Yesu. Amina. 

Ee Mt. Yosefu Mfanyakazi, leo tunakuja mbele yako, tukiomba kwa maombezi yako tujaliwe (………...Hapa taja Ombi lako)

Baba Yetu x 3 Salaam Maria x 3 Atukuzwe Baba x 3 


SIKU YA PILI

Mt. Yosefu, ulimwokoa na kumhudumia Neno wa Mungu, na chakula cha uzima kilichoshuka kutoka mbinguni. Uwaangalie mapadri wa Kanisa, ambao asili yao ni nyumba uliyoiongoza, na uwaombee ili nao pia, waweze kuwahudumia kwa uvumilivu watu waliowekwa chini ya uangalizi wao. Tunaomba mapadri wawafundishe kiaminifu waamini Neno la Mungu na kuumega mkate, wa uzima kila siku, kwa ajili yao.Tunaomba wawaimarishe katika imani na matumaini, wakiwafariji katika magumu na katika nyakati za kukukatisha tamaa. Pia umuombe Yesu wetu awavishe taji kwa kazi zao na utumishi wao kwake hapa duniani kwa kuwashirikisha uzima wa milele pamoja nawe Mbingguni milele na milele. Amina 

Ee Mt. Yosefu Mfanyakazi, leo tunakuja mbele yako, tukiomba kwa maombezi yako tujaliwe (………...Hapa taja Ombi lako)

Baba Yetu x 3 Salaam Maria x 3 Atukuzwe Baba x 3 


SIKU YA TATU

Mt. Yosefu Mwenyeheri, sala zako zinaweza kufanya mambo yasiyowezekana, yakawezekana. Tunakuomba uje kutusaidia katika shida na magumu tuliyonayo sasa. Uweke kwenye ulinzi wako shida na mahangaiko yetu tunayoyaleta kwako na utuombee, ili tuweze kupata msaada kadiri ya mapenzi ya Mungu. Baba yetu mpendwa, tunakutegemea kabisa, na kwa imani, tunajikabidhi kwako kama watoto wadogo waliyolala mikononi mwa baba zao. Isisemekane kamwe, kwamba tumekuomba bila mafanikio. Yesu na Maria hawawezi kukukatalia chochote unachowaomba. Kwa matumaini hayo, tunakuomba udhihirishe wema na Upendo wako mkubwa kama ilivyo nafasi yako kwa mchumba wako, Bikira Maria, na Mwanao Yesu. Amina 

Ee Mt. Yosefu Mfanyakazi, leo tunakuja mbele yako, tukiomba kwa maombezi yako tujaliwe (………...Hapa taja Ombi lako)

Baba Yetu x 3 Salaam Maria x 3 Atukuzwe Baba x 3


SIKU YA NNE

Mpendwa Mt. Yosefu, wewe ni msimamizi wa familia ya kanisa. Mungu alikuteua uwe kiongozi na mlinzi wa Familia Takatifu ya Nazareti. Ulichagua kufanya kazi ya useremala, amabayo iliwafanya baadhi ya watu waulizane juu ya Yesu wakisema; “Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii? Huyu si mwana wa seremala?” Tunaomba kwa sala zako, uwabariki na kuwatia moyo mafundi seremala wote ambao kazi zao ni sawa na ya kwako. Amina 

Ee Mt. Yosefu Mfanyakazi, leo tunakuja mbele yako, tukiomba kwa maombezi yako tujaliwe (………...Hapa taja Ombi lako)

Baba Yetu x 3 Salaam Maria x 3 Atukuzwe Baba x 3


SIKU YA TANO

Mt. Yosefu, Mwenyeheri, mume wa Bikira Maria, uwe nasi katika siku hii ya leo. Ulimlinda na kumthamini Bikira Maria. Ukimpenda mtoto Yesu kama mwanao wa kumzaa, ulimwokoa kutoka katika hatari ya kifo. Ulilinde Kanisa, nyumba ya Mungu, lililokombolewa kwa damu ya Yesu. Mlinzi wa familia Takatifu, uwe nasi katika majaribu. Tunaomba utuombee tujaliwe nguvu ya kuziepuka dhambi na kuzishinda nguvu za dhambi ili katika maisha tuweze kukua katika utakatifu na baada ya kufa, tuvikwe taji la ushindi na kufurahia milele na milele. Amina. 

Ee Mt. Yosefu Mfanyakazi, leo tunakuja mbele yako, tukiomba kwa maombezi yako tujaliwe (………...Hapa taja Ombi lako)

Baba Yetu x 3 Salaam Maria x 3 Atukuzwe Baba x 3 


SIKU YA SITA

Ee Mt. Yosefu, ambaye ulinzi wako ni mkubwa, wenye nguvu na wa haraka mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, tunakukabidhi mahitaji na haja za mioyo yetu. Ee Mt. Yosefu utusaidie kwa maombezi yako yenye nguvu na utuombee kwa Mungu atupatie Baraka zote za kiroho kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, ili kwa nafasi yako Mbinguni tuweze kumsifu na kumheshimu Baba Yetu wa milele. Ee Mt. Yosefu, kamwe hatutachoka kukufikiria wewe ukiwa umembeba Yesu, akiwa amelala mikononi mwako. Hatuthubutu kumsogelea akiwa amepumzika hivyo karibu na moyo wako. Tunakuomba umguse kwa kwa niaba yetu, umbusu, umuombe nae atubusu wakati tutakapovuta pumzi yetu ya mwisho. Mt. Yosefu, msimamizi wa wanakufaa, utuombee. Amina

Ee Mt. Yosefu Mfanyakazi, leo tunakuja mbele yako, tukiomba kwa maombezi yako tujaliwe (………...Hapa taja Ombi lako)

Baba Yetu x 3 Salaam Maria x 3 Atukuzwe Baba x 3 


SIKU YA SABA

Ee Mt.Yosefu, mfano wa wote wanojituma kufanya kazi, utujalie neema ya kufanya kazi kwa moyo wa toba kwa malipizi ya dhambi zetu nyingi; kufanya kazi kwa bidii kwa kuweka mbele upendo wa kufanya kazi; kuliko vionjo vyetu; kwa shukrani na furaha, kuona ni heshima kutumia na kukuza zawadi tulizopewa na Mungu, kwa njia ya kufanya kazi kwa utaratibu, amani na kwa kiasi na uvumilivu, pasipo kulegea kwa uchovu, au ugumu wa kazi; zaidi ya yote, kwa nia njema kabisa na kujikana wenyewe, tukikumbuka daima kifo na maelezo tunayotakiwa kuyatoa kwa muda tuliopoteza, talanta tulizofukia, mema amabyo hatujayatenda na kujiona sana katika mafanikio, kitu ambacho ni hatari katika kazi ya Mungu. Yote kwa Yesu, Yote kwa Maria, yote kufuata mafano wako, ee Baba wa imani Mt. Yosefu! Hii itakuwa ndio kaulimbiu yetu maishani mwetu na milele.

Amina

Ee Mt. Yosefu Mfanyakazi, leo tunakuja mbele yako, tukiomba kwa maombezi yako tujaliwe (………...Hapa taja Ombi lako)   

Baba Yetu x 3 Salaam Maria x 3 Atukuzwe Baba x 3 


SIKU YA NANE

Ee Yosefu mwenye heri, tunakimbilia kwako katika masumbuko yetu; na kisha omba shime ya Mchuma wako mtakatifu tunaomba pia kwa matumaini usimamizi wako. Kwa ajili ya mapendo uliyompenda Bikira mtakatifu mzazi wa Mungu, na kwa ajili ya kumtunza mtoto Yesu, twakuomba sana, utuangalie kwa wema siye tuliokuwa fungu lake Yesu Kristo, tukakombolewa kwa damu yake. Tusimamie katika masumbuko yetu kwa enzi na shime yako. Ee mlinzi amini wa jamaa takatifu, uwakinge watoto wateule wa Yesu Kristo. Ee baba uliyetupenda mno tuepushe na kilema chochote cha madanganyo na upotevu. Ee kinga yetu mwezaji, utusimamie huko juu mbinguni ulipo, tunaposhindana na wenye nguvu wakaao gizani. Kama vile siku za kale ukamwopoa mtoto Yesu katika hatari ya kuuawa, na leo hivi likinge kanisa takatifu la Mungu katika mitego ya adui, na katika shida yote, Mtunze daima kila mmoja wetu kwa mfano wako, ili tupate msaada wako, kukaa na utakatifu maisha, kufa kifo chema, na kupata mbinguni makao ya raha milele. Amina 

Ee Mt. Yosefu Mfanyakazi, leo tunakuja mbele yako, tukiomba kwa maombezi yako tujaliwe (………...Hapa taja Ombi lako)

Baba Yetu x 3 Salaam Maria x 3 Atukuzwe Baba x 3 


SIKU YA TISA

Mt. Yosefu, ututazame, sisi tuliyekuchagua wewe leo hii uwe msimamizi watu wakati wa uhai wetu na katika saa ya kufa kwetu. Ututazame na kutu zidishia moyo wa sala na wa kumtumikia Mungu. Ufukuze mbali nasi kila aina ya dhambi, utuombee ili kifo kisitujie tukiwa hatujajiandaa, bali tupate muda wa kutubu dhambi zetu zote kwa njia ya sakramenti ya kitubio katika hali ya majuto kamili, ili saa ile ya kufa kwetu tukabidhi roho zetu mikononi mwa Yesu na Maria. Amina. 

Ee Mt. Yosefu Mfanyakazi, leo tunakuja mbele yako, tukiomba kwa maombezi yako tujaliwe (………...Hapa taja Ombi lako) 

Baba Yetu x 3 Salaam Maria x 3 Atukuzwe Baba x 3 

SALA YA MWISHO

Ee bwana wetu Yesu kristo, tunaleta maombi yetu maalum kwako ingawa hayatimizi kamwe kwa ukamilifu mahitaji yetu na matamanio mengi yaliyomo moyoni mwetu. hatuombi kutimiziwa tu maombi yetu hayo bali Neema ya kukutegemea wewe katika kutimiza kiu ya mahitaji na matamaniao ya mioyo yetu ulivyotupatia wewe. Tunakuomba Bwana Yesu ujibu sala na maombi ya waja wako walioungana nasi katika kusali Novena hii. Tunakuomba uwabariki kwa pendo lako na uwatakatifuze. Tunakuomba kwa mioyo yetu iliyo wazi kabisa tukijua kuwa haitatufaidia chochote tukivipata vya ulimwengu huu na kuipoteza nafsi zetu. Ee bwana Yesu Kristu, tusaidie daima kuona wema na utukufu wako katika majaribu yetu yote. Tusaidie pia kuona Baraka zako kila siku na daima kukupenda zaidi na zaidi. Asante bwana Yesu kwa kila kitu kwetu. Amina.

Post a Comment

Previous Post Next Post