Masomo ya Misa 28/10/2024

Somo la Kwanza

Efe 2:19-22

Tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu. Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni. Katika yeye jengo lote linaungamanishwa vema na kuku ahata liwe hekalu takatifu katika Bwana. Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja kuwa maskani ya Mungu katika Roho.

Neno la Bwana, Tumshukuru Mungu 

Wimbo wa Katikati

Zab 19:1-4

Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu,

Na anga laitangaza kazi ya mikono yake.

Mchana husemezana na mchana,

Usiku hutolea usiku maarifa.

(K) Sauti yao imeenea duniani mwote.

Hakuna lugha wala maneno,

Sauti yao haisikilikani.

Sauti yao imeenea duniani mwote,

Na maneno yao hata miisho ya ulimwengu.

Katika hizo ameliwekea jua hema.

(K) Sauti yao imeenea duniani mwote.

Shangilio

Shangilio

Aleluya, aleluya,

Ee Mungu, tunakusifu, tunakukiri kuwa Bwana. Jamii tukufu ya Mitume inakusifu.

Aleluya.

Somo la Injili

Lk 6:12-16

Yesu aliondoka akaenda mlimani ili kuomba, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu. Hata kulipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake; akachagua kumi na wawili miongoni mwao, ambao aliwaita Mitume; Simoni, aliyemwita jina la pili Petro, na Andrea nduguye, na Yakobo na Yohane, na Filipo na Bartolomayo, na Mathayo na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Simoni aitwaye Zelote, na Yuda wa Yakobo, na Yuda Iskariote, ndiye aliyekuwa msaliti.

Neno la Bwana, Sifa kwako Ee Kristu 

Post a Comment

Previous Post Next Post