MAFUNGU YA ROZARI

Matendo ya furaha (Jumatatu na Jumamosi)
  1. Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa mama wa Mungu, Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
  2. Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti, Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani. 
  3. Yesu anazaliwa Bethlehemu, Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara.
  4. Yesu anatolewa Hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.
  5. Maria anamkuta Yesu Hekaluni. Tumombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.

Matendo ya uchungu (Jumanne na Ijumaa)
  1. Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu, Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
  2. Yesu anapigwa mijeledi kwa ajili yetu, Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
  3. Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu, Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.
  4. Yesu anachukua msalaba kwa ajili yetu, Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
  5. Yesu anakufa msalabani, Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.

Matendo ya utukufu (Jumatano na Jumapili)
  1. Yesu anafufuka, Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu
  2. Yesu anapaa mbinguni, Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni
  3. Roho mtakatifu anawashukia Mitume, Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
  4. Bikra maria anapalizwa mbinguni, Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri. 
  5. Bikra Maria anawekwa Malkia mbinguni, Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.

Matendo ya mwanga (Alhamisi)
  1. Yesu anabatizwa Mto Yordani, Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
  2. Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana, Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya injili.
  3. Yesu anatangaza ufalme wa Mungu, Tumwombe Mungu atujalie kupokea ufalme wake kwa toba ya kweli.
  4. Yesu anageuka sura, Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
  5. Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristi takatifu, Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.

               Tumsifu Yesu Kristo...

Post a Comment

Previous Post Next Post